• March 29, 2024

NDOA NDOANA (utamu ndani ya uchungu)

Ya mgambo ikilia ina jambo basi sasa imeshalia na mdharau biu hubiuka mwenyewe. karibu katika makala ya NDOA NDOANA tukiangazia maisha ya ndoa , yaani utamu ndani ya uchungu. Sisemi kitu.

Tukiyafungua macho na kutazama kwa undani hali ya ndoa miaka ya jadi, ndoa iliheshimika, ikatunzwa na watu wakaienzi. Tunapopiga jicho vitabu vya dini yayo hayo yanasisitizwa. Ndoa imekuwa kama biashara, ama nifananishe na siasa hasa za taifa la Kenya, lakini haya yanaishia tu hapa. Watu wanaingia watakavyo saa yoyote, wakati wowote kama vile mja anavyoingia msalani. Kwa maana nyingine ndoa imepoteza maadali na misingi yake thabiti. Tazama vile vijana wanavyokimbilia ndoa, utadhani kuna raha huko, badaaye wanatoka wakiwa na makovu ya moyo na hapo ndio utasikia “ALL MEN ARE DOGS” wengine watasema “ALL LADIES ARE THE SAME”. Wakati wengine wanazikimbia huku wengine wanazikimbilia.

Usikose kusikiliza makala haya. Mwelekezi ni Thomas Odhiambo, mimi naitwa Carrilus Mwangome nikishirikiana na Bosco Kathima.

Read Previous

DRAMA GALORE AS KPL TEAMS FAIL TO HONOR BETWAY SHIELD CUP ROUND OF 16 MATCHES

Read Next

Linguistics

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Most Popular